IMAGINE INGEKUWAJE KAMA ISINGEKUWEPO VALENTINE'S DAY TAREHE 14 FEBRUARY.

Siku ya wapendanao au maarufu kama VALENTINE'S DAY ni siku ya kushangaza sana.kila mtu ana fikra tofauti kuhusu maana halisi ya siku hii na chanzo cha siku hii.Tukianza kuzungumzia chimbuko la siku hii tutakua tunaingilia mada nyingine ndefu sana..Siku hii kuna watu wanaoihusudu na wapo wengine wanaoiona wala haina maana kwao.Pia ni siku ngumu sana kusherekea kwa watu  ambao hawako kwenye mahusiano yani single Boys na Single Ladies. Huwa najiuliza sana,Siku hii isingekuwepo je? Dunia ingekuwaje labda? bila siku hii ya wapendanao.

TUNGEONESHA VIPI UPENDO KWA WATU TUNAOWAPENDA

Kama ilivyo tuna siku 365 katika mwaka.inakuwaje ipo siku moja tu ya wapendanao? siku moja tu ya kuonesha upendo kwa watu tunaowapenda? Vipi kuhusu kuonesha jinsi gani tunawapenda watu kila siku ya maisha yetu?,yani siku zote 365? Is it possible? Inaweza kuwa ngumu lakini inabidi kujitahidi kuwaonesha jinsi gani tunawapenda wenzetu siku zote bila kujali uwepo wa Valentine's day..
 
wenyewe wanasema"Kila siku ni siku ya wapendanao kama upo kwenye mahusiano ya kweli"

NI LINI TUNGEPOKEA  ROSES? 

Siku hii utaona watu wakipeana maua waridi(roses) kuliko siku nyingine zote,kuna wenzangu na mimi siku hii tu ndo siku pekee tunapata maua kutoka kwa wapenzi wetu.
Kumsuprise mpenzi wako na maua au kitu chochote kizuri ni jambo ambalo linamfanya mtu kujiona ana thamani na kufeel upendo,,Kwa ambao wanafanyiwa hivi na wapenzi wao wanaelewa nachosema.Tuache utamaduni huu mbovu wa kusubiri valentines day ndo tupeleke maua kwa wapenzi wetu jamani.

JE NI LINI WAPENDANAO WANGEPASWA KUPEANA ZAWADI?

mwanzoni nilitangulia kusema kuwa tuna siku 365 katika mwaka,Guess what? unaweza kuchagua siku yoyote katika mwaka ukamsurprise mpenzi wako na bonge la zawadi na sio kusubiri tarehe 14 February.Fikiria kumpatia kipenzi chako zawadi siku yoyote katika mwaka.

SHUGHULI ZIPI TUNGEFANYA SIKU HII?

Good question... Tarehe 14 February isingekuwa valentines day ingekua siku tu ya kawaida kama siku nyingine,tungeendela na shughuli zetu za kila siku mfano kazi,biashara zatu na mambo mengine.Je tungeshindwa?

JE INGEKUWA VIGUMU?

Kutokana na jinsi watu tulivyozoea ingekua vigumu,lakini nachojaribu kusema hapa ni kwamba,Valentines day sio siku pekee ya kuonesha jinsi gani tunawapenda na kuwajali wapenzi wetu.Tusisite kuonesha upendo siku yoyote tu na sio kusubiri tarehe 14 February.


Una maoni gani kuhusu hili? Valentines day or not?


Share on Google Plus

About dr.joh health and wellness

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment